Wednesday, August 14, 2013

“Madiwani wa CCM Kagera waendelee na kazi”

 
 
 
 
 
 
Rate This

NAPE 1

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera jana tarehe 13/08/2013 katika kikao chake cha siku moja kilichofanyika mjini Bukoba imetangaza uamuzi wake wa kuwafutia dhamana ya CCM hivyo kuwavua Udiwani Madiwani wanane wa Manispaa ya Bukoba waliotokana na CCM.
Kwa mujibu wa utaratibu wa kutoa adhabu kwa viongozi wa CCM walio kwenye vyombo vya dola hasa Wabunge na Madiwani uamuzi wa Halmashauri Kuu ya Mkoa sio wa mwisho. Uamuzi huo unapaswa kupata Baraka za Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ndipo utekelezwe.
Hivyo basi, mpaka sasa Madiwani hao wanane waliosimamishwa wanapaswa kuendelea na kazi zao kama kawaida wakisubiri kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa kitakachoketi tarehe 23 Agosti, 2013 mjini Dodoma ambacho pamoja na mambo mengine kitapitia uamuzi huo wa Halmashauri Kuu ya Mkoa wa Kagera.
Pamoja na hilo, tumepokea barua za Madiwani hao za kukata rufaa kupinga uamuzi huo wa Halmashauri Kuu ya Mkoa kwa msingi wa madai ya kukiukwa kwa utaratibu katika kufikia uamuzi huo.
Tunawasihi wananchi wa Bukoba na Kata husika, wanachama na viongozi wote kuwa watulivu katika kipindi hiki ambapo suala hili linashughulikiwa na vikao vya Kitaifa.
Imetolewa na:
Nape M. Nnauye,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA
ITIKADI NA UENEZI
14/08/2013

FOLENI YA KWENDA KUMUONA SHEKH PONDA HOSPITAL YA MUHIMBILI


 
 
 
 
 
 
1 Vote

kkk
Waumini wa dini ya Kiislaa na watu wengine mbali mbali wakisubiri kuingia kumona Sheikh Ponda, alipolazwa hospitali ya Muhimbili Dar Es Salaam.

Keita ashinda uchaguzi wa urais Mali


Ibrahim Boubacar Keita ana jazi ngumu ya kukarabati nchi ya Mali
Ibrahim Boubacar Keita ameibuka mshindi wa uchaguzi mkuu nchini Mali huku mpinzani wake akikubali kushindwa katika duru ya pili ya uchaguzi wa urais.
Soumaila Cisse,amekubali kushindwa na mpinzani wake,aliyekuwa waziri mkuu Ibrahim Boubakar Keita.
Bwana Cisse aliyewahi kuhudumu kama waziri wa fedha amempongeza Keita kwa ushindi huo na kumtakia kila la kheri.
Bwana Keita, mwenye umri wa miaka 68, alihudumu kama waziri mkuu kutoka mwaka 1994 hadi 2000.
Mali imekumbwa na vurugu kwa kipindi cha mwaka mmoja ikiwemo mapinduzi ya kijeshi na kufuatiwa na harakati za jeshi la Ufaransa kuwaondoa wapiganaji waliokuwa wameteka eneo la Kaskazini mwa nchi.
Hata hivyo hakuna matokeo rasmi yametolewa kufuatia duru ya pili ya uchaguzi iliyofanyika Jumapili.
Katika duru ya kwanza bwana Cisse alipata 19% dhidi ya bwana Keita aliyepata 40%
Bwana Keita anayejulikana kama (IBK) - atakuwa na jukumu la kusimamia zaidi ya dola bilioni 4 za msaada wa kigeni kwa taifa hilo ambalo uliahidiwa kwa ukarabati wa nchi.
Umoja wa mataifa umeanza kupeleka kikosi cha wanajeshi 12,600 kitakachokuwa na jukumu la kudhibiti hali nchini Mali, huku wanajeshi wa Ufaransa wakianza kuondoka.
Baada ya duru ya kwanza ya uchaguzi Bwana Cisse alikuwa amelalamika kuwepo visa vya rushwa au ununuzi wa kura huku kura zaidi ya laki nne zikisemekana kuharibika.
Hata hivyo, mahakama ya kikatiba ya Mali ilikataa madai hayo huku kiongozi wa waangalizi wa Ulaya Louis Michel, akisifu uchaguzi huo kwa ulivyoandeshwa kwa njia ya uwazi.
Mnamo Jumatatu, waangalizi kutoka Muungano wa ulaya na muungano wa Afrika, walisifu ambavyo duru ya pili ya uchaguzi ilivyoendeshwa.
'Raia wa Mali wanapaswa kupongezwa kwa sababu kulingana na mimi ninavyoona, wanatii demokrasia,'' alisema Michel.
Kabla ya uchaguzi huo Bwana keita aliahidi kuleta maridhiano nchini humo iwapo angechaguliwa.
Makubaliano yaliyoafikiwa ili kuruhusu uchaguzi kuendelea katika eneo hilo la kazkazini yanashinikiza serikali iliyochaguliwa kuanzisha mazungumzo ya amani na waasi wa kundi la Tuareg katika kipindi cha miezi miwili.

44 wauawa kinyama msikitini, Nigeria

 
Maiduguri ni moja ya majimbo yaliyowekewa sheria ya hali ya hatari
Takriban waumini 44 wameuawa kwa kupigwa risasi wakiwa msikitini Kaskazini Mashariki mwa Nigeria, kwa mujibu wa maafisa wa jimbo la Borno.
Mauaji hayo yalifanyika wakati wa maombi ya asubuhi Jumapili , ingawa taarifa zimejitokeza Jumatatu , kutokana na hitilafu ya mawasiliano kwani jimbo hilo liko chini ya sheria ya hali ya hatari.
Shambulizi lilifanyika katika mji wa Konduga, ulio umbali wa kilomita 35 kutoka mji mkuu wa jimbo hilo , Maiduguri.
Washambulizi wanasemekana kuwa wanachama wa kundi la wapiganaji la Boko Haram, ambalo liliwaua maelfu ya watu tangu mwaka 2009.
Gazeti la Daily Post, liliripoti kuwa watu wengine 26 walikuwa wanatibiwa kwa majeraha waliyopata wakati wa shambulizi hilo hospitalini Maiduguri.
Mwanachama wa kikundi cha vijana kinachotoa ulinzi kwa raia, aliambia shirika la habari la Associated Press, kuwa wapiganaji wao wannne waliuawa walipojaribu kutoa kilio cha kutaka usaidizi.
Raia wengine kumi na wawili, waliuawa katika kijiji cha Ngom kinachopakana na Maiduguri.
Rais Goodluck Jonathan alitangaza sheria ya hali ya hatari katika majimbo matatu Kaskazini Mashariki mwa nchi mnamo mwezi Mei wakati wanajeshi walipofanya operesheni dhidi ya wapiganaji wa kiisilamu.
Boko Haram linapigania eneo la Kaskazini mwa nchi likitaka kujitawala kwa kutumia sheria za kiisilamu.
Mwandishi wa BBC mjini Lagos, anasema kuwa wakati kundi hilo limekuwa likishambulia makanisa, pia limekuwa likishambulia misikiti.
Habari za mashambulizi hayo zilijitokeza wakati kanda ya video ya kiongozi wa kundi hilo Abubakar Shekau, ilipotolewa akidai kundi hilo kuhusika na mashambulizi hayo ikiwemo kushambulizi dhidi ya vituo vya polisi na kambi za jeshi.

Taarfa zaidi Bbc swahili

Balaa Misri: zaidi ya 15 wauwa

Moto wawaka Misri
Zaidi ya watu kumi na watano wameripotiwa kuuwawa wakati maafisa wa usalama nchini Misri walipoanza operesheni ya kuwatimua wafuasi wa rais aliyeng'olewa madarakani Mohammed Morsi, waliokuwa wamekita kambi mjini Cairo.
Maandamano nchini Misri
Lakini vuguvugu la Undugu wa Kiislamu, Muslim Brotherhood, ambalo linaunga mkono maandamano hayo limesema idadi ya waliouwawa inazidi kumi na watano.
Milipuko ya risasi ilisikika na magari ya kivita yametumika kuwatimua waandamanaji hao.
Maafisa wa usalama walifyatua gesi ya kutoa machozi.
Maafisa wamesema kuwa kambi ya waandamanaji hao katika Medani ya Nahda magharibi mwa mji wa Cairo imevunjwa na waandamanaji kutawanywa.
Wizara ya mambo ya ndani imesema kuwa operesheni ya kusafisha barabara za mji huo inaendelea. Wanaharakati wanaomuunga mkono bwana Morsi walifukuzwa hadi hifadhi ya wanyama pori iliyopo karibu pamoja na chuo kikuu cha Cairo, kituo cha televisheni kinachomilikiwa na serikali Nile TV kimesema.

Sunday, August 11, 2013

Uamsho kumshitaki Sheikh Soraga

Sheikh Farid Ahmed Hadi, mmoja wa viongozi wa Uamsho walioko ndani.
Sheikh Farid Ahmed Hadi, mmoja wa viongozi wa Uamsho walioko ndani.
ZANZIBAR. Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) inakusudia kumfikisha katika vyombo vya sheria Katibu wa Mufti Zanzibar, Sheikh Fadhil Suleiman Soraga, kutokana na kuishutumu Jumuiya hiyo kuhusika na tukio la kuwamwagia tindikali mabinti wawili raia wa Uingereza.
Amir Haji, mlezi wa Jumuiya hiyo, alisema wamesikitishwa na taarifa zilizotolewa katika magazeti mbali mbali ya hapa nchini likiwemo Tanzania Daima, Mtanzania, Zanzibar Leo na Uhuru yaliyomnukuu Sheikh Soraga huyo kuihusisha Uamsho kuhusika na tukio hilo.
“Uislamu unakataza kufanya mambo maovu kwa kujidhuru mwenyewe au mtu mwengine aliye Muislamu na asiyekuwa Muislamu”, alisema Amir Haji na kuongeza kuwa mara nyingi Jumuiya hiyo imekuwa ikipakwa matope kuhusishwa na uovu kama huo ilhali haina malengo hayo.
“Cha kusikitisha zaidi ni kiongozi Muislamu kusema maneno kama hayo ya kutupaka matope. Shutuma hizi zimezidi mipaka na ndugu yetu Sheikh Soraga amelipalia makaa. Kila siku tunapakwa matope. Lakini tunamuomba kama hana la kusema basi anyamaze na kama ana ushahidi basi autoe katika vyombo vya sheria na sheria ichukue mkondo wake“, alisema Amir Haji, ambaye pia amemtaka Katibu huyo wa Mufti  kuwaomba radhi Waislamu na jumuiya hiyo.
Kwa upande wake Katibu wa Uamsho, Said Hamad, ameishauri serikali kufanya uchunguzi wa kina wa kubaini wahalifu waliotenda unyama wa kuwamwagia tindikali wasichana wawili wa Kiingereza, Kirstie Trup na Katie Gee, wote wenye umri wa 18, na kuwachukulia hatua za kisheria ili kukomesha vitendo hivyo kuendelea hapa nchini.
Katibu huyo wa Uamsho aliwataka wananchi kutoa ushirikiano wa kina kwa jeshi la Polisi nchini ili kufanikisha uchunguzi juu ya tukio hilo.
Uamsho yalalamikia watoto wa masheikh kutokuruhusiwa kuwaona baba zao

Wizi ulitokea wakati moto unawaka

Askari polisi saba wanahojiwa na wachunguzi nchini Kenya, wakishukiwa kuhusika na uporaji wakati wa moto ambao uliteketeza eneo la mapokezi la uwanja wa kimataifa mjini Nairobi mwanzo wa juma.
Sehemu ya uwanja wa ndege wa Nairobi iliyoteketea

Askari hao, akiwemo inspector, wanashutumiwa kuiba pesa na ulevi.
Wafanyakazi wa uwanja wa ndege, uhamiaji na madereva wa taxi ni kati ya wale wanaohojiwa, baada ya kamera za usalama kuonesha watu wakiiba vitu madukani.
Wakuu piya wanawatafuta watu wane waliokuwa wakisubiri kufukuzwa nchini kabla ya moto huo kutokea.
Watu hao wametoweka.
Ijumaa Rais Uhuru Kenyatta alisema moto huo haukutokana na kitendo cha kigaidi.