MUSIC

 BUNGE LAAHIRISHWA TENA LEO MPAKA UFUMBUZI WA GESI MTWARA UTAKAPOJULIKANA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Anna Makinda ameliahirisha tena bunge leo asubuhi ili kupisha kamati ya uongozi ya Bunge iendelee kukutana ili kutoa maamuzi na tamko kuhusu vurugu za Mtwara zilizojotokeza jana na kusababisha mtu mmoja kufariki dunia na uharibifu mbalimbali kutokea ikiwemo kuchomwa moto nyumba za viongozi wa serikali,chama cha mapinduzi na nyumba ya mwandishi wa habari wa TBC.
Pia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini umesimamishwa kwa muda mpaka ufumbuzi wa tatizo la vurugu hizo utakapopatiwa suluhisho.

Kesho bajeti ya makadirio ya mapato na matumizi ya Afrika Mashariki itajadiliwa.
 

How to tell if the IRS is eyeing you

4 hours ago
A general view of the Internal Revenue Service (IRS) Building in Washington, May 14, 2013.
Reuters
A general view of the Internal Revenue Service (IRS) Building in Washington, May 14, 2013.
You consider yourself a law abiding citizen, and you are not starting a nonprofit organization with conservative ties.
Even so, you may be a candidate for a tax audit—and you may have no clue what you have done to warrant the attention of the IRS.
The nation's tax collectors have long made it a practice to look for discrepancies, omissions and suspicious activity to uncover tax evasion and fraud. And lately, the IRS has expanded its monitoring to include social media.
The agency now keeps an eye out for online discussions about nonpayment or underpayment of taxes, and even sale prices of goods on sites like eBay that don't match what taxpayers report.
In a world where companies like Amazon can keep tabs on consumers' online activities, the shift by the IRS is reasonable, says Edward Zelinsky, a law professor at Cardozo Law School. "This was always known to people in the tax community that the IRS, like everybody else in the 21st century, was monitoring online."
But Zelinsky is just one expert concerned about the lack of transparency around the IRS' practices. The agency "is so secretive about what is going on that that really erodes public confidence," he said.
(Read More: IRS Mess Could Yield Tax Reform: Baucus)
The American Civil Liberties Union has also expressed qualms about IRS secrecy. That group filed a Freedom of Information Act request for documents explaining whether the IRS always obtains search warrants to read email and other electronic communications. "Unfortunately, while the documents we have obtained do not answer this question point blank, they suggest otherwise," wrote Nathan Freed Wessler, a staff attorney at the ACLU.
So how can you know if you are under scrutiny? You can't know exactly, but some moves are more likely than others to attract attention.
Noncash deductions are a prime example, according to several tax experts. If you donate a car to the American Lung Association, or a large quantity of clothing to the Salvation Army, make sure that the deduction you take is reasonable, and that you can document how you came to that amount.
(Read More: Obama: Miller Out as Acting Commissioner of IRS)
Taxpayers who are self employed often appear to face more scrutiny as well. "If you are in business for yourself, or you work for someone who is, know that the IRS is watching," Frederick W. Dailey III, a tax lawyer and the author of "Stand Up to the IRS," said on his website.
The IRS also keeps an eye out for cash-based businesses, and for mismatches between what others file about you and what you file. For example, if you neglect to include a payment for some freelance work during the year, and the payer reports that as a business expense, you are likely to get some scrutiny. This would also hold true if you neglect to report gains from an investment account, and the investment firm reports them.
Wealthier taxpayers seem to be more likely to get chosen for audit, perhaps because that gives the IRS a greater chance to recover significant sums. (Every year the government collects only about 83 percent of what it is owed, a gap of several hundred billion dollars at a time when the budget deficit is a flashpoint.)
According to IRS data, taxpayers making $1 million or more are more than 12 times more likely than the rest of the population to be examined. In 2010, about one in 100 Americans were audited. The IRS audited 3.8 percent of returns for those making $200,000 or higher, versus 12.5 percent of returns for those making $1 million or more.
As for the online monitoring, Zelinsky says it may be simply the application of new tools to old agency search standards. So while he is deeply frustrated by the IRS' lack of transparency, he added, "If they are using social media to find cash based businesses, or looking for phony medical deductions or the other hot buttons, then I would applaud that."
There is no surefire way to prevent an audit. But experts say one practice definitely improves your odds: Don't do what the IRS does. Be open. About everything.
The agency declined to comment about this story.

POLISI 7 WATIWA MBARONI KWA KOSA LA " KUWATIA VIJITI MATAKONI " WATUHUMIWA NA KUSABABISHA VIFO


POLISI saba kutoka wilayani Kasulu, wamepandishwa kizimbani katika Mahakama Kuu Kanda ya Tabora, iliyoanza kikao chake mjini Kigoma leo na kusomewa mashitaka ya kuua kwa kukusudia. 
 
Mbele ya Jaji Sam Rumanyika, askari Polisi hao walidaiwa kuwa Agosti 6, 2011 walimpiga na kumuua kwa makusudi Festo Stephano, mkulima na mkazi wa Kijiji cha Rungwe mpya wilayani Kasulu mkoani Kigoma.


Waliopandishwa kizimbani na kusomewa mashitaka yao ni pamoja na Baraka Hongdi, Koplo Mawazo, Koplo Swahib, Koplo Charles, Koplo Shamsi, Koplo Jerry na Koplo Amrani ambao kwa pamoja walikana mashitaka.
 
Baada ya kukana mashitaka, kesi hiyo ilianza kusikilizwa kwa mashahidi wa upande wa Jamhuri kuanza kutoa ushahidi wao, ambapo shahidi wa kwanza katika kesi hiyo, Masumbuko Stephano, aliieleza Mahakama kwamba askari hao walikusudia kufanya mauaji hayo.
 
Masumbuko aliieleza Mahakama kwamba siku ya tukio, alikamatwa pamoja na marehemu na mgambo wa kijiji, na kuwekwa katika mahabusu ndogo katika Ofisi ya Mtendaji wa Kata.
Alidai baada ya kufika, askari hao walianza kuwapiga kwa kutumia vitako vya bunduki, fimbo na chupa za bia, hali iliyosababisha wapatwe na maumivu makali.
Shahidi huyo alidai kuwa baada ya kupigwa na kukaribia kupoteza fahamu, polisi hao waliwavua nguo, wakawafunika na turubai ndani ya gari ambapo baadaye walinunua magunia ya mkaa na kuwakandamiza na magunia hayo.
 
Shahidi wa pili katika kesi hiyo, Andrea Sama, alidai kwamba askari hao walikusudia kufanya mauaji siku hiyo, kwani licha ya kutoa kipigo pia waliwavua nguo na kuwaingiza miti kwenye sehemu zao za haja kubwa.

“Mheshimiwa Jaji kwa kweli nilishuhudia vitendo vya askari hao kwa macho yangu, na nilishindwa kuamini kama jambo hilo linafanyika kwenye ardhi ya Tanzania au tuko nchi nyingine, maana unyama uliofanywa na askari polisi hao huwezi kudhani kama ni walinzi wa amani katika nchi hii,” alidai Sama.


Kesi hiyo itaendelea kusikilizwa mfululizo hadi kutolewa hukumu, ambapo mwanasheria mwandamizi wa Serikali, Juvelin Rugaihuruza, alidai kuwa upande wa Jamhuri ambao ndiyo mlalamikaji, unatarajia kuwa na mashahidi 12 na vielelezo viwili.
 
Washitakiwa hao wanatetewa na Mwanasheria, Method Kabuguzi, kutoka Kampuni ya Uwakili ya Kigoma Law Chamber and Advocate ya mjini Kigoma.
 May 15 2013

Somalia yapiga hatua kufungua upya balozi zake.

Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa anafanyia kazi kufunguliwa upya kwa balozi na ujumbe wa kidiplomasia ambazo zilikuwa zimefungwa tangu mwaka 1991, katika juhudi za kufungamanisha uhusiano wa nchi za nje na serikali mpya ya shirikisho ya Somalia.
  • Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud (kati) akiweka tufali la saruji katika eneo la ubalozi mpya huko Doha, Qatar, mwezi Machi. Waziri wa Mambo ya Nje Fowsiyo Yusuf Haji Aadan na maafisa wa Qatar wakiangalia. [Jalada] Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud (kati) akiweka tufali la saruji katika eneo la ubalozi mpya huko Doha, Qatar, mwezi Machi. Waziri wa Mambo ya Nje Fowsiyo Yusuf Haji Aadan na maafisa wa Qatar wakiangalia. [Jalada]
  • Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud (kushoto) na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ubelgiji Didier Reynders wakishikana mikono huko Brussels mwezi Januari. [Na Bruno Fahy/AFP] Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud (kushoto) na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ubelgiji Didier Reynders wakishikana mikono huko Brussels mwezi Januari. [Na Bruno Fahy/AFP]
Katibu Mkuu wa wizara hiyo Mohamed Sharif Mohamud alisema kuwa Somalia inayo mipango ya kufungua upya karibuni balozi zake duniani kote, akizitaja za Marekani, Uingereza, Ufaransa, Japan, Algeria na Iraq.
Kwa kuteuliwa kwa Rais Hassan Sheikh Mohamud mwezi Septemba 2012 na kuimarika kwa hali ya usalama nchini Somalia, nchi zimeanza kufungua upya balozi zao mjini Mogadishu vilevile, zikiwemo Uingereza, Misri, Kenya, Nchi za Falme za Kiarabu na Iran. Nchi nyengine nyingi zenye uhusiano wa kidiplomasia na Somalia zina wajumbe zao mjini Nairobi.
Wizara pia itawaondosha baadhi ya mabalozi kwa uteuzi ambao utafungamana bora zaidi sera za serikali za uchumi na maendeleo ya binadamu, Mohamud alisema.
Utawala wa Mohamud ulianza kutekeleza mabadiliko mwezi Machi, wakati Ubalozi wa Somalia ulipofunguliwa upya mjini Brussels, ili kutoa huduma kwa Wasomali waliomo katika Jumuiya ya Ulaya.
Hapo tarehe 18 Aprili, serikali ya Somalia ilimteua Abdullahi Mohamed Ali kama mjumbe wake wa kidiplomasia huko London; anatarajiwa kuwasilisha rasmi vitambulisho vyake kwa serikali ya Uingereza hivi karibuni.

Mabadiliko ya Kidiplomasia

Mohamed Osman Mohamed, mshauri wa masuala ya kisiasa katika Ubalozi wa Somalia huko Juba, Sudan ya Kusini, alisema kuwa kiasi cha mabalozi 15 na wakuu wa ujumbe kutoka nchi za Kiarabu, Kiafrika na Ulaya wataitwa upya. Alionya, hata hivyo, mchakato wa kuwarejesha maafisa hawa unahitaji kiwango kikubwa cha mawasiliano ili kuepuka kuwachanganya wanadiplomasia wanaoondoka.
Mchambuzi wa masuala ya kisiasa Hamdi Khalif Bashir alisema kwamba hapo januari, Wizara ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa ilianza mchakato wa kuwaita upya wakuu wa ujumbe wa kidiplomasia ambao muda wao ulikuwa umemalizika.
"[Serikali ya kijeshi ya Mohamed Siad Barre] ilifungua balozi 40 na balozi ndogo tano zikiwemo balozi za Tunisia, Nigeria, Senegal, Serbia, Sweden na nchi nyengine kadhaa," aliiambia Sabahi.
"Serikali ya sasa ya shirikisho hata hivyo, imeteua mabalozi wapya na mabalozi wadogo ili kuamsha sera mpya za kigeni," Bashir alisema na kuongeza kuwa wizara inatafuta waajiriwa wenye angalau miaka miwili ya uzoefu wanaoweza kuzungumza lugha kadhaa.
Aliwatia moyo wanasiasa wanaondoka kumaliza kipindi chao kwa wema. Ninawaomba wanadiplomasia wote wa Somalia wawe watu wa haki na kujitenga na tabia ya kuwa kila kitu kitakwenda vibaya na kukata tamaa," alisema. "Wanapaswa kufanya kazi ya kulinda amani na kufuata njia ya mafanikio ili waweze kutuma ujumbe wa uhuru, haki na upendo."
Waziri wa Mambo ya Nje Fowsiyo Yusuf Haji Aadan atapendekeza majina kwa baraza la mawaziri ili kupigiwa kura. Kwa mujibu wa katiba, rais ana uwezo wa mwisho kwa uteuzi rasmi.
May 15 2013

Somalia kuchukua udhibiti wa anga mwaka huu

Serikali ya Somalia itachukua udhibiti wa anga lake mwishoni mwa mwaka 2013, alisema Waziri wa Habari, Posta na Simu Abdullahi Ilmoge Hirsi siku ya Jumatatu (tarehe 13 Mei).
"Tumekubaliana kwamba serikali ya shirikisho ya Somalia (itakuwa) tayari kuchukua majukumu yake ya udhibiti wa eneo lake la anga kufikia tarehe 31 Disemba 2013," alisema Hirsi baada ya mkutano na wawakilishi kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa na Mamlaka ya Kusimamia Anga ya Somalia yenye makao yake Nairobi (CACAS), iliripoti Redio RBC ya Somalia.
Umoja wa Mataifa ulichukua jukumu la kusimamia anga la nchi hiyo miaka 19 iliyopita kufuatia kuanguka kwa serikali kuu ya Somalia, ikafungua CACAS mwaka 1996 kwa ajili ya kukusanya mapato ya ndege zinazoruka kupitia anga hilo kwa niaba ya Somalia.
Zaidi ya wafanyakazi 100 wa usimamizi wa anga watahamishwa na kupelekwa Mogadishu katika matayarisho ya kipindi hicho cha mpito, na wafanyakazi wa ndani watapewa mafunzo katika kipindi cha mwaka kilichobakia.


May 15 2013
Waandamanaji waachilia nguruwe kwenye maandamano juu ya madai ya fedha ya wabunge wa Kenya.
Waandamanaji nchini Kenya waliwaachia nguruwe dazeni mbili kwenye milango ya bunge siku ya Jumanne (tarehe 14 Mei), wakamwaga damu kwenye sakafu wakilalamikia madai ya kupandishwa sana kwa mishahara ya wabunge wapya.
  • Mwandamanaji mmoja akiwa ameinama karibu na nguruwe kwenye milango ya bunge tarehe 14 Mei wakati wa maandamano jijini Nairobi dhidi ya wabunge waliodai mishahara mikubwa. [Simon Maina/AFP] Mwandamanaji mmoja akiwa ameinama karibu na nguruwe kwenye milango ya bunge tarehe 14 Mei wakati wa maandamano jijini Nairobi dhidi ya wabunge waliodai mishahara mikubwa. [Simon Maina/AFP]
"Hatutawaruhusu wabunge kujiongezea mishahara tukiwatazama tu," alipiga mayowe aliyepanga maandamano, Okiya Omtatah, kwa mujibu wa shirika la habari la AFP. "Ni waroho kama walivyo hawa nguruwe tuliowaleta hapa."
Polisi waliwakamata watu 10, wakatumia gesi ya machozi kuwatawanya waandamaji na kuwapiga wengine kwa magongo. Kisha walikimbia nyuma ya nguruwe hao waliotanda kwenye eneo lenye majani linalozunguka jengo la bunge.
Mnamo mwezi Machi, Kamisheni ya Mishahara na Ujira (SRC) ilikata mshahara wa wabunge isiyokatwa kodi kutoka shilingi 851,000 (dola 10,100) kwa mwezi hadi shilingi 535,000 (dola 6,400).
Mithika Linturi, mbunge anayeunga mkono mswada wa kuifuta SRC, alisema waandamanaji hao walipaswa kutumia "njia muafaka kuwasilisha malalamiko yao."
"Kenya si taifa la ovyo ovyo. Eneo la bunge lazima liheshimiwe," alisema Linturi, akiongeza kwamba wabunge "wana haki ya kuwa na mawazo yao hata kama hayamfurahishi kila mtu."

No comments:

Post a Comment