Friday, December 28, 2012

Balozi Seif awafariji na kutoa mkono wa pole kwa wakristo kufuatiwa kujeruhiwa kw Padre Ambrose Mkenda

pole



 
 
 
 
 
 
Rate This

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alifika katika makazi ya padri Ambrose Mkenda wa Paroko wa parokia ya kanisa katoliki la Mpendae Zanzibar kuupa pole uongozi wa Kanisa hilo pamoja na Familia yake kufuatia ajali ya kupigwa risasi hivi karibuni na watu wasioujulikana.
Tukio hilo la kusikitisha lililofanywa na watu wawili waliopakiana kwenye Vespa lilitokea langoni mwa Skuli ya Francis Maria iliyopo Tomondo Wilaya ya Magharibi ambapo ndio makaazi ya Padri Ambrose.

Balozi Seif akiufariji Uongozi huo alisema ni jambo baya na la kusikitisha lililofanywa na watu hao ambalo limetoa sura mbaya kwa Taifa na Serikali kupitia vyombo vyake vya ulinzi itaendelea kufanya uchunguzi wa tukio hilo na haitasita kuwachukuliwa hatua za kisheria watu watakaobainika kufanya uhalifu huo.
Alisema Serikali imesikitishwa na kulaani kitendo cha watu hao ambacho kinaashiria uvunjifu wa amani pamoja na kuwaweka wananachi katika hali ya wasi wasi usio wa lazima ndani ya harakati zao za kimaisha.
Akitoa shukrani kwa niaba ya Uongozi na Familia ya Padre Ambrose Mkenda Kiongozi kutoka Kanisa la Roman Catholic Father Shayo aliiomba Serikali kuendelea kuimarisha ulinzi wa raia wema ili kupunguza hofu iliyotanda mioyoni mwao kutokana na matukio ya uvamizi.
Father Shayo alitahadharisha kwamba hulka mbaya iliyoanzishwa na baadhi ya watu kuwafundisha watoto wadogo tabia ya kukashifu watu wazima kwa sababu ya utofauti wa Kidini inawajengea maisha mabovu watoto hao. “ Watoto wadogo kufundishwa tabia ya kukashifu watu wengine tuelewe kwamba Taifa halitakuwa na muelekeo mwema wa jamii yake ya baadaye”. Alitahadharisha Father Shayo.
Na Othman Khamis Ame

Hukumu kesi ya Lema yaibua mapya

LEMA



 
 
 
 
 
 
Rate This

0
inShare

MWANAZUONI aliyebobea katika sheria, Profesa Issa Shivji na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Francis Stolla wamekosoa hukumu ya Mahakama ya Rufani, iliyomrejesha bungeni, Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti juzi, wanasheria hao walisema hukumu hiyo iliyotolewa na majaji watatu wakiongozwa na Nathalia Kimaro, Salum Massati na Bernard Luanda, inapingana na sheria.
Hata hivyo, mmoja wa mawakili wa Lema, Method Kimomogoro amepinga madai hayo akisema wanaoipinga pengine hawajapata nafasi ya kuliangalia kwa undani suala la haki ya mpiga kura kupinga matokeo mahakamani.
Profesa Shivji kwa upande wake alieleza kushangazwa na maelezo ya Mahakama ya Rufani kuwa mpiga kura hana haki ya kufungua kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi na kusema hiyo ni sawa na kutunga sheria mpya na si kutafsiri zilizopo.
Alisema Sheria ya Bunge ya Uchaguzi, Katiba ya nchi na Mahakama, vinampa haki mpiga kura kufungua kesi kupinga matokeo ya uchaguzi.
“Sheria ya Bunge na Mahakama Kuu katika kesi ya Mgonja (Chediel ya mwaka 1980), vinampa haki mpiga kura kufungua kesi mahakamani kupinga matokeo. Sijaona hoja nzito ya Mahakama ya kufuta haki hiyo ya mpiga kura,” alisema Profesa Shivji.
Katika shauri hilo namba 84 la mwaka 1980 lililofunguliwa na William Bakari na mwenzake dhidi ya Mgonja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Mahakama Kuu Tanzania iliamua kuwa, mpiga kura ana haki kufungua kesi mahakamani kupinga matokeo. Walalamikaji walishinda.
Hata hivyo, Mahakama ya Rufani katika kesi ya Lema, iliamua kwamba hukumu katika kesi ya Mgonja ilikosewa kwani si sahihi kwamba mtu yeyote bila kujali mahali alipojiandikisha na kupiga kura anaweza kupinga matokeo katika jimbo lolote nchini hata kama haki zake hazijakiukwa kwa namna yoyote.
Lakini Profesa Shivji aliitetea hukumu hiyo ya Mgonja akisema imekuwapo kwa zaidi ya miaka 30 sasa na kwamba kwa muda wote huo imekuwa ikifuatwa katika uamuzi wa mashauri mbalimbali, huku akisisitiza kuwa Mahakama haiwezi kuifuta kirahisi tu.
Profesa Shivji alisema mpiga kura ni mwananchi na kwa vyovyote ana masilahi katika uchaguzi husika na hivyo anatarajia kuona uchaguzi ambao ni huru na wa haki.
“Hivyo huwezi kusema hahusiki na nani kashinda au kashindwa kwa kuwa uchaguzi ni muhimu katika kujenga na kukuza demokrasia,” alisema Profesa Shivji. Chama cha Wanasheria
Kwa upande wake, Stolla alisema: “Nimesikiliza hata maoni ya wanasheria mbalimbali wakizungumzia kutofurahishwa na tafsiri ya Mahakama ya Rufani kuhusu haki ya mpiga kura ‘ku-challenge’ (kupinga) matokeo ya uchaguzi mahakamani,” alisema na kuongeza:
“Katika uamuzi wa kisheria, inaonekana Mahakama imetunga sheria mpya na wengi tunajiuliza kama siyo, sababu ya kuwa mpiga kura ni ipi nyingine inampa haki mpiga kura kupinga matokeo?”
Stolla alisema Sheria ya Bunge ya Uchaguzi ya tangu mwaka 1985, ambayo ilifanyiwa marekebisho mwaka 2002, kabla ya kutungwa upya mwaka 2005, inampa haki mpiga kura kupinga matokeo ya uchaguzi mahakamani.
“Mwaka 2002, sheria zote zilifanyiwa marekebisho na baadaye mwaka 2005, Bunge likatunga sheria mpya inayoitwa Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, ikafuta ya mwaka 1985. Sheria hiyo na marekebisho yake, ndiyo inayotawala uchaguzi hadi sasa,” alisema.
Alisema hata kabla ya kutungwa kwa sheria hiyo ya Uchaguzi ya mwaka 1985, tayari kulikuwa na uamuzi wa Mahakama Kuu katika kesi ya Mgonja ambayo iliamua kuwa mpiga kura ana haki ya kupinga matokeo ya uchaguzi mahakamani.
 CHANZO MWANANCHI

Mjadala waendelea kuhusu dhima ya serikali ya muungano nchini Tanzania


Na Deodatus Balile, Dar es Salaam

Dhima na muundo wa serikali ya muungano kwa mara nyingine tena vimechochea mjadala mkali miongoni mwa Watanzania wakati Tume ya Kupitia upya Katiba (CRC) ilifanya mfuatano wa mikutano na wananchi huko Zanzibar wiki iliyopita.
  • Rais wa visiwa vinavyojitawala kwa sehemu vya Tanzania Zanzibar Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na rais wa Tanzania Jakaya Kikwete wakati wa sherehe za Kikwete kuapishwa jijini Dar es Salaam tarehe 6 Novemba 2010. Zanzibar iliungana na Tanganyika bara mwaka 1964, na kuunda Tanzania. [Yasiyoshi Chiba/AFP] Rais wa visiwa vinavyojitawala kwa sehemu vya Tanzania Zanzibar Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na rais wa Tanzania Jakaya Kikwete wakati wa sherehe za Kikwete kuapishwa jijini Dar es Salaam tarehe 6 Novemba 2010. Zanzibar iliungana na Tanganyika bara mwaka 1964, na kuunda Tanzania. [Yasiyoshi Chiba/AFP]
Tume ilifanya mikutano 54 katika mkoa wa Mjini Magharibi wa Zanzibar kuanzia tarehe 19 Novemba hadi tarehe 18 Disemba kama sehemu ya jitihada zake za kukusanya maoni ya wananchi kuhusu katiba mypa, ambayo ilipangwa kujadiliwa na Mkutano wa Bunge mwezi Aprili 2014. Uchaguzi mkuu umepangwa kufanyika 2015.
Mikutano imekuwa ikifanyika Tanzania nzima tangu Julai, na raia kutoa maoni na malalamiko moja kwa moja kwa tume. Karibia raia 200,000 walihudhuria mikutano ya hivi karibuni huko Zanzibar, kwa mujibu wa mkuu wa Tume ya Kupitia upya Katiba Mwesiga Baregu.
Hata hivyo, licha ya kupenda kuhudhuria mikutano miongoni mwa wananchi kwa ujumla, Baregu alisema washiriki walio wengi walielewa visivyo mikutano ya kupitia katiba na kura ya maoni ya wananchi kuhusu kama serikali ya muungano iwepo au isiwepo.
"Kwa bahati mbaya, Wazanzibari walio wengi wanafikiri fursa hii ya kukusanya maoni ya wananchi kwa ajili ya kuandika katiba mpya ya Tanzania ilikuwa ni fursa ya kutathmini muungano, lakini haikuwa hivyo," aliiambia Sabahi.
Visiwa vya Zanzibar viliungana na Tanganyika bara mwaka 1964 kuunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika mchakato huo, serikali ya Tanganyika ilivunjwa, lakini Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ilibakizwa kuwepo pamoja na serikali mpya ya muungano iliyoundwa.
Katika katiba ya sasa, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayojitawala kwa sehemu ina mamlaka ya kisheria katika mambo ya ndani, wakati serikali ya muungano wa kitaifa inadhibiti sera ya hazina ya serikali, mambo ya nje, jeshi na ulinzi, madaraka ya dharura, uhamiaji, madeni na biashara ya taifa.
Salim Hassan Khamis, mwenye umri wa miaka 55, mzaliwa wa Zanzibar aliyehudhuria mkutano katika Jimbo la Magomeni, alisema viongozi wanapaswa kuelewa kwamba wananchi wa Zanzibar wanataka kuwa na uzito sawa wa kisiasa kama bara. "Kama ilivyo, unaposema muungano [serikali], inaeleweka kuwa serikali ya Tanganyika," aliiambia Sabahi.
Khamis alisema baadhi ya watu wanafikiri kwamba kwa sababu Zanzibar ni ndogo kuliko Tanganyika, inapaswa kunyenyekea ndani ya muungano. Lakini hiyo ni hoja isiyohitajika, alisema, kwa sababu Zanzibar ilikuwa ni taifa huru kabla ya kuungana na Tanganyika ambayo nayo ilikuwa huru.
Deus Kibamba, mwanasheria na mkurugenzi mtendaji wa Dawati la Habari za Raia Tanzania, alisema aina ya serikali iliyopo imepitwa na wakati.
Kibamba alisema viongozi katika ngazi mbalimbali za serikali hawafuati mipaka ambayo imeelezwa katika makubaliano ya muungano ambayo inaeleza wazi ni wizara zipi na sekta za viwanda zilizo katika jukumu la serikali ya muungano na ni zipi zilizoachwa kusimamiwa kipekee na serikali za ndani ya Zanzibar na bara.
Alisema kwa mfano, serikali ya muungano kwa sasa inaigharimia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ambayo inahusika na bara tu na sio Zanzibar.
Alisema tatizo lilianza wakati serikali mbili zilipoungana pamoja, wakati asasi za serikali ya Tanganyika zilipoingizwa katika serikali ya muungano bila ya kufuata kanuni kuhusu mamlaka ya kisheria au kushughulikia kujirudia kwa dhima na mahitaji ya bajeti.
Kibamba alisema suluhisho linalowezekana linaweza kuhusisha kurejesha serikali ya Tanganyika na kuanzisha bunge la jamhuri ambapo waziri mkuu angewakilisha serikali ya muungano na kila nchi ingekuwa na rais wake mwenye madaraka machache.
Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu anayehusika na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa George Mkuchika alisema maoni ya raia yalikuja kwa wakati, kwa kuwa madhumuni ya tume ni kuchambua mawazo yao na kuwasilisha matokeo yake kwa taifa kwa ajili ya kujadiliwa.
Alisema mchakato wa kuandika katiba unahusisha kupiga kura ya kukubali au kupinga mawazo na kuwahamasisha Watanzania kuendelea kuzungumza wazi bila ya woga. "Jambo pekee ninaloweza kusema ni kwamba raia wote wana haki ya kutofautiana mawazo, lakini watafikia muafaka wa jinsi tunavyotaka katiba yetu iwe kupitia masanduku ya kura," aliiambia Sabahi.

Wapiganaji 5 wa al-Shabaab waasi huko Baidoa


Desemba 27, 2012
Wapiganaji watano wa al-Shabaab wameasi na kujiunga na vikosi vya serikali ya Somalia huko Baidoa, Redio Daljir ya Somalia iliripoti Jumanne (tarehe 25 Disemba).
Kamanda wa Polisi wa Bay Mahad Abdirahman alisema waliokuwa wanachama wa al-Shabaab wataweza kurekebishwa, akiongeza kwamba utawala huo unatarajia wapiganaji zaidi kuasi na kujiunga na vikosi vya serikali.
Uasi huo ulitokea baada ya Jeshi la Taifa la Somalia kuzidisha operesheni zake dhidi ya al-Shabaab katika mkoa wa Bay, kwa mujibu wa kamanda wa mkoa Kanali Mahad Abdirahman.
Waziri wa Mambo ya ndani na Usalama wa Taifa Abdikarim Hussein Guled Jumanne alitoa sharti la mwisho la siku 100 kwa wapiganaji wa al-Shabaab kujisalimisha na kujiunga na mchakato wa amani.

Al-Shabaab yajikusanya upya huko Bulo Burde kabla ya shambulio kubwa


Na Majid Ahmed, Mogadishu

Desemba 27, 2012


Al-Shabaab wanajaribu kujikusanya huko mkoa wa Hiran wa Somalia baada ya kukabiliwa na mfululizo wa kushindwa na kupoteza miji ya kimkakati mmoja baada ya mwengine katika miezi ya hivi karibuni, maafisa wa usalama wa Somalia wasema.
  • Askari wa Jeshi la Taifa la Somalia wakiwa wamepumzika kwenye kivuli cha mti huko Jowhar tarehe 11 Disemba baada ya kuukamata mji uliokuwa unashikiliwa na al-Shabaab kwa msaada wa majeshi ya Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia. [Na Stuart Price/AU-UN IST/AFP] Askari wa Jeshi la Taifa la Somalia wakiwa wamepumzika kwenye kivuli cha mti huko Jowhar tarehe 11 Disemba baada ya kuukamata mji uliokuwa unashikiliwa na al-Shabaab kwa msaada wa majeshi ya Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia. [Na Stuart Price/AU-UN IST/AFP]
Ahmed Abdullahi, afisa wa usalama katika mkoa wa Hiran, alisema kuwa alipokea habari ya harakati ya baadhi ya viongozi wakuu wa al-Shabaab wanatoroka kutoka maeneo yaliyokombolewa na kuelekea Bulo Burde.
"Kwa mujibu wa kile ambacho tumeambiwa na wakaazi wa Bulo Burde baadhi ya viongozi wa al-Shabaab kama vile Yusuf Sheikh Isse, amabaye ni dhamana wa mkoa wa Shabelle ya Kati, na viongozi wengine wamekuwa wakija mji huu," Abdullahi aliiambia Sabahi.
"Tangu vikosi vya washirika vilipoukamata mji wa Jowhar, makamanda wa vita wa kikundi hicho wamekuwa wakiondoka kutoka maeneo ya Shabelle ya Kati na kuelekea Hiran ya mashariki," alisema na kuongeza kuwa vikosi vya Somalia na Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) vinajitayarisha kuelekea Bulo Burde.
"Jeshi la Taifa la Somalia, kwa msaada wa vikosi vya AMISOM, vimekuwa katika tahadhari na viko tayari kuikomboa miji michache iliyobakia katika makucha ya al-Shabaab, ikiwemo Bulo Burde," alisema.
Bulo Burde, ambao uko kilomita 240 kaskazini ya Mogadishu na kilomita 40 kusini mashariki ya Beledweyne, inachukuliwa kuwa ni ngome ya mwisho imara ya al-Shabaab huko Hiran.
Kwa mujibu wa wakaazi, mamia ya wapiganaji wa al-Shabaab wamejificha mjini humo, wakijitayarisha kuukinga baada ya kupoteza udhibiti wa miji mingi ya maeneo ya kusini na kati ya nchi.
Kikundi hicho cha wanamgambo kilitangaza wiki iliyopita kuwa kimeunda kikosi kimoja kipya kinachojulikana "Kikosi cha Abu Yahya al-Libi", kinachoitwa hivyo kwa jina la kiongozi wa al-Qaida ambaye iliripotiwa kuwa aliuliwa mapema mwaka huu huko Pakistani.
Tarehe 17 Disemba, al-Shabaab iliwaonesha wanachama wa kikosi hicho kipya katika shughuli iliyofanyika huko Bulo Burde kama juhudi za kuwapanga upya wapiganaji wake walioshindwa, kwa mujibu wa taarifa za habari.
Hata hivyo, jaribio la al-Shabaab kujikusanya upya linakabiliwa na vikwazo vingi kutokana na mizozo ya ndani inayoendelea baina ya uongozi wa al-Shabaab pamoja na matatizo ya kifedha ya kikundi hicho, wachambuzi wa masuala ya usalama wasema.
"Al-Shabaab imepoteza maeneo ya kimkakati ambayo yalikuwa yakileta mapato kama vile Mogadishu na Kismayu, kwa hivyo haitaweza kupata fedha za kutosha kujipanga yenyewe na kugharamia operesheni zake za kijeshi," alisema Mohamed Ali Mohamed, kepteni mstaafu wa Idara Usalama wa Taifa la Somalia.
Al-Shabaab haitaweza kulinda Bulo Burde, Mohamed alisema. Kinyume chake, wapiganaji watarudi nyuma na kuelekea misituni baina ya mikoa ya Shabelle ya Kati na Hiran kwa ajili ya kujikinga, alisema.
"Kama ambavyo tulivyoona katika miezi iliyopita, wapiganaji wa al-Shabaab wamekuwa wakirejea nyuma kutoka miji yote bila ya ushindani mara tu vikosi vya washirika vinapokaribia," aliiambia Sabahi.
"Kujitoa kwa Al-Shabaab kutoka miji ya kimkakati kuelekea maeneo ya vijijini hakumaanishi kuwa wamechagua kutojihusisha na vita ili kuepuka kupata hasara kubwa," alisema. Maana yake ni kwamba kikundi hakiwezi kuhimili mashambulizi na kuyakinga maeneo yaliyo katika udhibiti wao, kwa hivyo wanachama wake hukimbilia maeneo ya vijijini kwa kujilinda."

Al-Shabaab inawalazimisha watoto kubeba silaha

Wakaazi wa eneo la Bulo Burde walisema kwamba al-Shabaab imewateka nyara watoto na kuwalazimisha kubeba silaha katika juhudi ya kukinga mashambulizi kutoka Jeshi la taifa la Somalia na majeshi ya AMISOM.
"Al-Shabaab imewakamata watoto wasiopungua 150 kutoka shule na madrasa ya Qur'an ambao wametekwa kutoka kote nchini na vijiji vidogo vinavyoizunguka Bulo Burde," mkaazi Abdinur Dahir mwenye umri wa miaka 46, aliiambia Sabahi.
"Viongozi wa al-Shabaab akiwemo Sheikh Yusuf Ali Ugas, afisa wa kikundi hicho katika mkoa wa Hiran region, pamoja na viongozi wengine sasa wapo mjini," alisema. "Wanawataka walimu katika shule za Qur'an na shule za kawaida kusitisha masomo yao na kuwapeleka wanafunzi wao kwenye kambi za mafunzo ili waweze kujifunza jinsi ya kutumia silaha na kujiunga na kikundi hicho katika vita vyake vya jihadi, kama wanavyodai."
Nasra Abdi, mwenye umri wa miaka 42, anayeuza maziwa safi katika soko la mji, alisema aliwaona wanachama wa al-Shabaab mitaani, wakiwataka wakaazi kujiunga na kikundi hicho ili kuulinda mji dhidi ya shambulio linalotarajiwa kutoka vikosi vya Somalia na washirika.
"Kikundi hiki ni adui wa watu wa Somalia kwa sababu ya vitendo vyao dhidi ya watu wasio na hatia, hasa vijana ambao wanalazimishwa kubeba silaha na kupigana kwa ajili hao," alisema.