Sunday, December 2, 2012

WAHAMIAJI WAPO HATARINI ZAIDI KUAMBUKIZWA UKIMWI

Wahamiaji wako hatarini zaidi kuambukizwa Ukimwi: IOM

Kusikiliza / Hamishia
Shirika la kimataifa la Uhamiaji, IOM limesema wahamiaji wanaathirika zaidi na virusi vya ukimwi na Ukimwi hususan katika nchi zenye vipato vya juu.
IOM inasema kuwa ripoti ya mwaka huu ya UNAIDS inaonyesha kuwa kwa mara kwanza katika historia ya Ukimwi, maambukizi mapya ya ugonjwa huo katika nchi zilizokuwa na mzigo mkubwa wa maambukizi hayo yanapungua, lakini bado kuna changamoto.
Ripoti hiyo inatoa mfano wa nchi zenye vipato vya juu kama zile za Amerika Kaskazini na Ulaya ambako inasema idadi ya watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi imeongezeka katika kipindi cha miaka Kumi iliyopita.
Imesema wahamiaji na watu wanaohamahama wako hatarini zaidi kuambukizwa virusi hivyo kwa sababu mipango mingi ya afya huwaengua mara kwa mara na hata hawawezi kupata huduma za afya. Jumbe Omari Jumbe ni msemaji wa IOM
((SAUTI YA JUMBE OMARI JUMBE)

ZANZIBAR HEROES WAPIGWA 2-0


Zanzibar Heroes yalala kwa Malawi 2 – 0, yatinga robo fainali CECAFA

Wachezaji wa Zanzibar Heroes

Wachezaji wa Zanzibar Heroes
Timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes, leo hii imefungwa 2-0 na timu ya taifa ya Malawi katika mchezo wa mwisho wa kundi C katika mchezo uliopigwa katika uwanja wa Wankulukuku. Magoli ya Malawi yalifungwa mapema ambapo Ndaziona Tchasalia aliweka kimioni bao la kwanza dakika ya 3 baada ya mchezo kuanza huku goli la pili likifungwa na Chuikepo Msowoya katika dakika ya 6 ya mchezo huo.
Licha ya kujaribu kusawazisha, Zanzibar Heroes  ilijikuta ikikabiliana na ukuta mgumu wa timu ya Malawi ambayo pia imefanikiwa kuingia katika Robo fainali kwa kumaliza na pointi sita.
Hata hivyo, Zanzibar Heroes nayo imeweza kufuzu kuingia robo fainali kutokana na kuwa “best loser” kwa kuweza kupata pointi nne katika mechi zake mbili za awali dhidi ya Eritrea na Rwanda.
Itapambana na Burundi siku ya Jumatatu saa 10.00 jioni katika mchezo unaotarajiwa kutoa upinzani mkali kwani Burundi haijapoteza kupoteza hata mchezo mmoja katika kundi lake huku Zanzibar ikijaribu kukumbuka historia yake ya kuweza kulinyakua kombe la CECAFA mwaka 1995 katika nchi ya Uganda.