Sunday, December 2, 2012

ZANZIBAR HEROES WAPIGWA 2-0


Zanzibar Heroes yalala kwa Malawi 2 – 0, yatinga robo fainali CECAFA

Wachezaji wa Zanzibar Heroes

Wachezaji wa Zanzibar Heroes
Timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes, leo hii imefungwa 2-0 na timu ya taifa ya Malawi katika mchezo wa mwisho wa kundi C katika mchezo uliopigwa katika uwanja wa Wankulukuku. Magoli ya Malawi yalifungwa mapema ambapo Ndaziona Tchasalia aliweka kimioni bao la kwanza dakika ya 3 baada ya mchezo kuanza huku goli la pili likifungwa na Chuikepo Msowoya katika dakika ya 6 ya mchezo huo.
Licha ya kujaribu kusawazisha, Zanzibar Heroes  ilijikuta ikikabiliana na ukuta mgumu wa timu ya Malawi ambayo pia imefanikiwa kuingia katika Robo fainali kwa kumaliza na pointi sita.
Hata hivyo, Zanzibar Heroes nayo imeweza kufuzu kuingia robo fainali kutokana na kuwa “best loser” kwa kuweza kupata pointi nne katika mechi zake mbili za awali dhidi ya Eritrea na Rwanda.
Itapambana na Burundi siku ya Jumatatu saa 10.00 jioni katika mchezo unaotarajiwa kutoa upinzani mkali kwani Burundi haijapoteza kupoteza hata mchezo mmoja katika kundi lake huku Zanzibar ikijaribu kukumbuka historia yake ya kuweza kulinyakua kombe la CECAFA mwaka 1995 katika nchi ya Uganda.

No comments:

Post a Comment