Saturday, December 1, 2012

USHAIRI

Kulikumba Jini

Kulikumba Jini
Utumwa naliopewa, nende kwa jini nifike
Hamshike sawasawa, nimfunge afungike
Ashindwe jipapatuwa, chupani nimfundike
Kisha nende panganikwe, silisili kumtia
Na vifaa nikapewa, na nyenzo za uhakika
Makombe hazinguliwa, ya kunywa na ya kupaka
Na kafara hasomewa, na hirizi hajivika
Alipo nikamfika, lengo kwenda mchukuwa
Halikuta kubwa jini, lisilo mfano wake
Tangu juu hadi chini, sioni khatima yake
Katikati msituni, ‘meketi kitini pake
Bali nisitetemeke, nili nikijiamini Read the rest of this entry

Ningekuwa Sikupendi

Ningekuwa Sikupendi
Ningekuwa Sikutaki
Ningekuwa sikutaki, sege nawe ‘singekaa
Nisingefanya dhihaki, usoni ningekwambia
‘Singejipatisha dhiki, wala ‘singeng’ang’ania
Lakini n’nabakia, sababu nakuashiki
‘Ngekuwa sikuhitaji, kale ningeshakwachia
‘Singekufaya mkwiji, nendapo nakuchukua
Hawa hayapiti maji, bilawe kukuwazia
Sababu ya yote haya, wewe kwangu kama taji
Ningekuwa sikupendi, siri ‘singekufanyia
‘Singeupiga umundi, na boso na tarazia
Kusema halinishindi, wazi nikakuwekea
Lakini nawe wajua, mapenzi hayana fundi
Read the rest of this entry

U Wapi Ewe Furaha?

U Wapi Ewe Furaha?
Ninakujua Furaha hu mja wa kusalia
Hu mja unayekaa daima ukabakia
Huja mara ukangia na mara ukapotea
Lakini hebu rejea! Read the rest of this entry

No comments:

Post a Comment