Friday, December 28, 2012

Wapiganaji 5 wa al-Shabaab waasi huko Baidoa


Desemba 27, 2012
Wapiganaji watano wa al-Shabaab wameasi na kujiunga na vikosi vya serikali ya Somalia huko Baidoa, Redio Daljir ya Somalia iliripoti Jumanne (tarehe 25 Disemba).
Kamanda wa Polisi wa Bay Mahad Abdirahman alisema waliokuwa wanachama wa al-Shabaab wataweza kurekebishwa, akiongeza kwamba utawala huo unatarajia wapiganaji zaidi kuasi na kujiunga na vikosi vya serikali.
Uasi huo ulitokea baada ya Jeshi la Taifa la Somalia kuzidisha operesheni zake dhidi ya al-Shabaab katika mkoa wa Bay, kwa mujibu wa kamanda wa mkoa Kanali Mahad Abdirahman.
Waziri wa Mambo ya ndani na Usalama wa Taifa Abdikarim Hussein Guled Jumanne alitoa sharti la mwisho la siku 100 kwa wapiganaji wa al-Shabaab kujisalimisha na kujiunga na mchakato wa amani.

No comments:

Post a Comment