Monday, December 10, 2012

Huduma mpya ya barua-pepe kwa simu za mikononi yaiva Somaliland

Kazi ya kutoa huduma ya barua-pepe kwa watumiaji milioni moja wa simu za mkononi imekamilika, maafisa wa kampuni ya Telesom ya Somaliland wameiambia Sabahi.
  • Mtumiaji wa Telesom akitembea katika mitaa ya mji wa Hargeisa. Huduma mpya itaunganisha huduma za ujumbe wa maneno na barua pepe. [Barkhad Dahir/Sabahi] Mtumiaji wa Telesom akitembea katika mitaa ya mji wa Hargeisa. Huduma mpya itaunganisha huduma za ujumbe wa maneno na barua pepe. [Barkhad Dahir/Sabahi]
  • Jengo maarufu la Intaneti mjini Hargeisa ukiwa umefungwa kwa chakula cha mchana. Huduma mpya ya Telesom inawapa watumiaji fursa ya kupata barua-pepe kupitia simu zao za mikononi bila ya kutegemea migahawa ya intaneti. [Barkhad Dahir/Sabahi] Jengo maarufu la Intaneti mjini Hargeisa ukiwa umefungwa kwa chakula cha mchana. Huduma mpya ya Telesom inawapa watumiaji fursa ya kupata barua-pepe kupitia simu zao za mikononi bila ya kutegemea migahawa ya intaneti. [Barkhad Dahir/Sabahi]
Telesom inajitayarisha kuzindua huduma hiyo iliyokuwa imesubiriwa kwa muda mrefu wiki chache zijazo baada ya kuingia ubia na kampuni ya kimataifa ya Kimarekani inayojihusisha na shirika ya kimataifa ya tovuti na programu za kompyuta, Google, kutoa teknolojia hiyo, alisema mkuu wa idara ya kimataifa ya Telesom, Mohamud Haji Abdirahman.
Telesom iliingia kwenye ubia na Google hapo Aprili 2011 kutoa huduma hiyo mpya, ambayo itawaruhusu watumiaji wa Google kuwasiliana na wateja wa Telesom bure kupitia ujumbe mfupi wa maneno wa simu za mkononi.
Mwezi uliopita, mwakilishi wa Google kwa nchi za Afrika chini ya Jangwa la Sahara, Divan Lan, alivifanyia uchunguzi vifaa vya Telesom katika makao makuu ya kampuni hiyo, mjini Hargeisa, kabla ya uzinduzi huo.
Katika makubaliano ya ushirikiano wao, watumiaji wa Gmail wataweza kutuma barua pepe kwa nambari za simu za mkononi za Telesom ambazo zitawafikiwa watumiaji wa Telesom kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno, alisema Abdirahman. Watumiaji hao wa simu nao wataweza kuzijibu barua hizo kwa kutumia ujumbe mfupi wa maneno.
Abdirahman alisema kuzigeuza barua pepe kuwa ujumbe mfupi wa maandishi kutawaruhusu watumiaji wa Telesom kuweza kutumia fursa za mtandao wa Intaneti kuwasiliana kwa ufanisi zaidi.
Jambo hili linawaweka huru watu kutoka ile dhiki ya kutafuta migahawa ya intaneti ambapo si kila mara hukuta kompyuta ya kutumia,” alisema. “Kwa huduma hii sasa, watumiaji wataweza kujibu haraka ujumbe wanaotumiwa kwa sababu wanaweza kuchukuwa simu popote pale.”
Huduma hii itakuwa na athari kubwa juu ya namna watu wanavyowasiliana kwa kazi na kwa burudani, alisema Abdi Osman Ali, mtaalamu wa teknolojia ya habari mjini Hargeisa. “Inaonesha maendeleo ambayo Somaliland imeweza kuyafikia katika eneo la [teknolojia ya] mawasiliano,” alisema.
Ubia wa Telesom na Google ni muhimu kwa sababu ambazo ziko juu ya zile za utumaji wa ujumbe wa maandishi kwa barua pepe, kwa mujibu wa mchumi, Abdirahman Aden Ismail.
Ismail anasema makubaliano hayo ni muhimu sana kwa sababu yanatengeneza kigezo kwa makampuni mengine makubwa ya kimataifa kuwekeza Somaliland. “Yanaweza kupelekea ubia wa Telesom na makampuni mengine makubwa ya kimataifa,” Ismail aliiambia Sabahi.
Telesom iliundwa mwaka 2001 na kundi la Wasomali, baadhi yao wanaoishi nje ya nchi, ili kutoa huduma pana zaidi za mawasiliano kwa watumiaji kwenye eneo hilo.
Abdirahman alisema kampuni hiyo ilikuwa ya kwanza kutoa huduma za simu ya mkononi nchini Somalia, ambayo inawawezesha wateja kutumia huduma ya kuhamishia simu zao wanapokuwa nje, miongoni mwa mambo mengine.
Mwaka jana, kampuni hiyo ilianzisha mtandao wa 3G huko Somaliland na sasa inawahudumia zaidi ya wakaazi milioni moja wa Somaliland, alisema.
Kampuni hiyo inatarajia kushirikiana tena na Google kuanzisha huduma za kuinua uchumi na hasa kushughulikia mahitaji ya sekta binafsi, alisema.

No comments:

Post a Comment