Saturday, December 1, 2012

DOLE WATAKA SERIKALI MBILI


Dole wataka Serikali Mbili

dole
Katika ukusanyaji wa maoni kwa ajili ya Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye jimbo la Dole asubuhi ya tarehe 1 Disemba 2012, waliotaka mfumo wa Muungano huu uliopo kati ya Tanganyika na Zanzibar uendelee kama ulivyo bila ya kufanyiwa marekebisho ni 115 na waliotaka Zanzibar na Tanganyika ziwe na Muungano utakaoiwezesha Zanzibar kuwa na mamlaka yake kamili ikifuatiwa na Muungano wa mkataba ni 5.  Tume ya Kukusanya Maoni ya wananchi jioni ya leo itakuwa shehia ya Kinuni, wilaya ya Magharibi Unguja.

No comments:

Post a Comment