Thursday, December 13, 2012

Mchango wa mawasiliano kwenye MKUZA


KATIBU MTENDAJI WA TUME YA UTANGAZAJI ZANZIBAR ND, CHANDE OMAR CHANDE
Katibu Mtendaji wa Tume ya Utangazaji Zanzibar, Chande Omar
Iwapo itatumika ipasavy, sekta ya mawasiliano inaweza kuwa na mchango mkubwa sana katika kuufanikisha Mpango wa Kitaifa wa Kupunguza Umasikini Zanzibar (MKUZA).
Hayo yameelezwa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Utangazaji Zanzibar, Chande Omar wakati akifungua semina ya siku mbili juu ya mkakati wa mawasiliano katika MKUZA katika ukumbi wa hoteli ya Bwawani.
Chande amesema kuwa elimu inahitajika kutolewa kwa wananchi kujua dira na dhamira ya serikali katika mpango huo ili kuweza kufikia mafanikio.
“Jamii inahitaji kupewa taarifa mbali mbali kupitia vyombo vya habari pamoja na mitandao ya kijamii ili kupata taarifa muhimu.“ Amesema Chande.
Naye Kamishna wa Ukuzaji Uchumi kutoka Wizara ya Fedha na Uchumi, Dk. Rahma Mahfoudh ameutolea ufafanuzi kuhusu MKUZA II juu ya kutokomeza umasikini Zanzibar.
Akizungumza katika ufunguzi wa semina hiyo Kamishna wa Mawasiliano Ikulu, Hassan Khatib, amesema kuwa kukosekana kwa uwelewa wa MKUZA kwa wananchi ni jambo linalokwamisha juhudi za serikali kufikia malengo yake ya kuondosha umasikini.

No comments:

Post a Comment