Thursday, December 13, 2012

Mimi ni muumini wa mfumo wa muungano uliopo’- Waziri Mwinyihaji Makame


WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapiznduzi, Dk Mwinyihaji Makame Mwadini
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapiznduzi, Dk Mwinyihaji Makame Mwadini
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapiznduzi, Dk Mwinyihaji Makame Mwadini, amesema kuwa, yeye ni muumini wa mfumo wa Muungano uliopo na sio Muungano wa mkataba kama baadhi ya wananchi wanavyotaka.
Alisema kuwa, katika hilo yeye hamumunyi mdomo, wala hapati kigugumizi na anaamini mfumo uliopo hivi sasa wa serikali mbili, ndio unaofaa kwa pande mbili za Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar.
Dk Mwinyihaji Makame Mwadini, alitumia fursa hiyo, kueleza hayo, huko katika ukumbi wa Misali Sunset Beach, Wesha Chake Chake Pemba, katika mkutano wa kikao cha tano cha ushirikiano, baina ya Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serekali za mitaa Zanzibar na wizara ya nchi ofisi ya waziri Mkuu tawala za mikoa na serikali za mitaa Tanzania bara.
Alikiri kuwepo kwa kero za Muungano ambapo, amesema kuwa zinafanyiwa ufumbuzi, na serikali zote mbili, na wala sio kuwepo kwa serekali ya mkataba kama wananchi wanavyodai.
“Mimi ni muumini wa Muungano wala hakuna Muungano wa mkataba kama baadhi ya wananchi wanavyodai katika sehemu mbali mbali”alisema Dk Mwinyihaji.
Alifahamisha kuwa, katika kushinda goli, lazima wananchi wadumishe Muungano, kudumisha udugu na kupiga vita adui ujinga na ukoloni mamboleo, sambamba na kuwataka wajumbe hao kusaidiana katika kujenga Zanzibar yenye amani na utulivu.
Aliongeza kuwa, katika kujenga nchi pamoja na kuendeleza elimu, mambo ya afya na huduma zote za kijamii kwa ustawi wa wananchi wao kama ilivyo lengo la vikao hivyo, ambavyo hujadili mada mbali mbali ambazo zitatoa mambo muhimu ambayo yatakayo wasaidia wananchi wotepamoja na kujua changamoto zinazowakabili katika ufanikishaji wa shuhuli zao.
Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serekali za mitaa Tanzania Bara ( ELIMU), Kassim Majaaliwa, alizitaka ofisi zote za bara na visiwani kulenga kutoa huduma bora kwa wananchi, hususana katika suala zima la elimu kwa watoto.
Alisema kuwa umefika wakati kwa wajumbe kuwa makini kuhakikisha wanatoa majibu mazuri, kama ililivyo lengo la serekali zote mbaili kuwahudumia wananchi wake kikamilifu na kuwatatulia kero zao.
“Niwajibu wetu kuyatekeleza hayo kwa wananchi, kwani wananchi wanatarajia kuona matunda mazuri kutoka katika kikao chetu hichi maalumu ambacho serikali nzima leo ipo hapa”alisema Naibu waziri Majaliwa.
Alifahamisha kuwa, kutokana na kuongezeka idadi ya watu, Rais Kikwete aliona ipo haja kwa kila kijiji kuweka shule ya msingi li kweza kuwapatia elimu watoto na kuwajengea mfumo mzima wamustakbali wa maisha yao ya baadae.
Naye Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Aggrey Mwanri, amesema kuwa, ziara hizozitawasaidia katika kudumisha Muungano, kwa kujenga umoja, amani na upendo kwa viongozi wa serikali na wananchi kwa ujumla.
Aliwataka wajumbe wa mkutano huo, kujenga umoja na mshikamano ambao utakaoweza kuwapatia malengo ambayo yatakayo weza kuwaletea ushindi katika kazi zao za baadae za kuwahudumia wananchi

No comments:

Post a Comment