Thursday, December 13, 2012

CHAMA cha soka Zanzibar ZFA kimeombwa kuwashirikisha na kuwa nao karibu wachezaji waliowahi kuwika zamani, ili kuchota taaluma ya kukuza soka hapa nchini.

Kisiwa cha Pemba
Kisiwa cha Pemba

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti wanandika hao wa zamani waliovuma na timu za Tamasha na Mkoani Shooting za Mkoani, walisema wanashangaa kuona ZFA haiwatumii katika masuala ya soka. Walisema kuwa wao wanayo mengi ya kukipa chama hicho, lakini wamekuwa hawashirikishwi katika mipango na mikakati yao, jambo ambalo linawashangaaza sana.
Salim Abdallah Kiburungu, alisema haoni kwamba ZFA inayoa azama na nia ya kweli ya kukuza kiwango cha soka hapa nchini, kutokana na kutokuwa na mipango ya kweli juu ya hilo.
Kiburungu ambaeo aliwahi kukipiga na timu ya taifa ya Zanzibar na Tanzania, alifafanua kuwa, ikiwa kweli ZFA inataka kuendeleza mbele soka na Zanzibar kutisha kama enzi zao, ni vyema kuzilazimisha timuz zote wanazoziongoza kuhakikisha wanakua na timu ndogo ndogo (vitalu)
‘’Sisi japo hazikuwa rasmi, lakini wakati wazee wetu wanacheza basi zilikuwepo timu ndogo ndigo na iwapo zile kubwa zinataka wachezaji basi kwanza wanaangalia zile zilizozpo na sio kuwenda kijiji chengine’’,alisema.
Ali Khamis Mtumweni ambae anae aliekuwa kuwa mchezaji wa timu ya faifa ya Zanzibar na Taifa Stars, alieleza kuwa pamoja na kwamba sasa ZFA inapata ufadhili kila wakati, lakini hado timu za Zanzibar zinapotoka nje ya Tanzania hazifanyi vyema.
Hivyo amekipa rai Chama hicho kuhakikisha kuwa, wanazinyanyua timu zilizoko madaraja madgo, kwani huko ndio vipaji vinakoanzia na sio kushughulikia timu kubwa ambazo zimechoka.
‘’ZFA kwa karne hii kama inadhamira ya kweli inaweza kukuza soka la Zanzibar, maana miundombinu inaruhusu sana lakini wengi wapo madarakani kwa maslahi yao binafsi na sio ya taifa hili’’,alifafanua Mtumweni.
Katika hatua nyengine Mshambuliaji huyo aliekuwa akikipiga na timu ya Tamasha ya Mkoani, aliwataka wachezaji kuwa na moyo wa kujitolea, uzalendo, uwajibikaji ili kuliletea heshima taifa hili.
Nae Foum Haji mchezaji wa zamani wa klabu hiyo ya Tamasha, alisema uwepo wa vilabu vyingi havinyanyui soka badala yake vimekuwa vikishushua soka kwani ushindani unaojitokeza hausaidii kwa taifa.
Hata hivyo alisema kwa sasa kama kweli vijana wanayonia ya kukuza soka na Zanzibar kuwa moto wa kuotea mbali, wanayonafanasi hiyo kutokana na miundombinua kuwa bora ikiwa ni pamoja na waalimu, wafadhili na maisha kuwa afadhali.
Hata hivyo amewataka wachezaji wa makocha wa kileo wasiache kuwatumia wao ili kuwapa mbinu na miongozo sahihi ya kufikia mafaniki yao katika soka

No comments:

Post a Comment