Saturday, December 1, 2012

POLISI AJERUHIWA ZNZ

Polisi ajeruhiwa kwa mapanga Zanzibar

Kamishna wa Polisi Zanzibar, Musa Ali Musa

Kamishna wa Polisi Zanzibar, Musa Ali Musa
Watu wasiojulikana wamemvamia askari polisi mmoja na kumjeruhi kwa mapanga, mnamo majira ya saa 10:00 alasiri katika huko Mboriborini kando kidogo ya mji wa Zanzibar. Imeripotiwa kwamba kundi hilo la watu lilimvamia askari huyo anayejulikana kwa jina la Othman Juma na kufanikiwa pia kuchukua pesa alizokuwa nazo ingawa haijajulikana ni kiasi gani mpaka sasa. Hatua za kumpatia matibabu askari huyo zinaendelea vizuri katika hospitali ya Al Rahma, Kilimani Unguja.

No comments:

Post a Comment